Where everything, and anything around YOU and me can be talked about...calling on all my fellow Africans...And if you don't like it, then put something you do like ...
Saturday, May 14, 2011
SHERIA ZA TAMASHA LA NYAMA CHOMA
SHERIA NA KANUNI ZA TAMASHA LA NYAMA CHOMA 2011.
1. Usafi na kanuni za afya lazima zizingatiwe kwa vyovyote, kutakuwa na afisa afya atayekagua mabanda yote na kuhakikisha vyakula vyote vinatayarishwa kwa hali ya usafi, endapo utakutwa unapuuzia hili, utatolewa kama mshiriki bila kurudishiwa kodi ya banda.
2. Mshiriki anatakiwa kufika kwenye tamasha na vitendea kazi vyote vya matayarisho, vikiwemo vyombo vya kuhifadhia chakula na vya kuuzia wateja.
3. Mshiriki haruhusiwi kuuza vinywaji vya aina yoyote ile.
4. Mshiriki anatakiwa aanze matayarisho ya uaandaaji na upishi masaa sita kabla, geti litafunguliwa saa 5 na nusu asubuhi, hivyo masaa sita kabla.
5. Mshiriki atazingatia usafi wakati wote wa tamasha, na atashiriki katika kuhakikisha banda lake limeachwa safi baada ya shughuli.
6. Mshiriki anatakiwa aahidi kuwa na uwezo wa kilo 60 za Nyama, ambacho ni kima cha chini, unaweza kuja na zaidi ya hiyo. KITIMOTO HAKIRUHUSIWI.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment